Siasa mchezo wa hovyo sana

              SIASA BANA
Inafahamika wazi na wengi tumeaminishwa kuwa siasa ni mchezo mchafu 

Kwa sasa hii iko wazi ukiangalia siasa zetu na viongozi wetu tanzania jinsi zinavyokwenda na jinsi mambo yanavyoendeshwa 

 Kama kuna kipindi ambacho vyama vya siasa vinatakiwa kuwa makini nikipindi hichi cha hama hama ya viongozi ambayo imekuwa ikisikika kila kukicha 

Watu wamepokea kwa hisia tofauti hamahama hii, wapo wanaodai kuwa kuhama kwa viongozi ni kudhofisha chama flani na kuimalisha kingine

Wengine wanasema hii nijanja janja ya chama ili kujua mbinu ya mpinzani wako lazima ukae karibu nae na ikiwezekana ule nae kabisa kwa lengo la kumwaminisha kuwa upo upande wake 

Kuna watu hawataki kabisa kuamini katika hayo yote wao wamejikita katika msimamo wa kuwa uoga na njaaa ndio chanzo cha wao kuweza kuhama kutoka chama kimoja kwenda  kingine

Lakini ukirudi nyuma ukasikiliza tamko alilolitoa aliekuwa mwenyekiti wa vijana Bavicha patrobas katambi kuhusiana na tukio la mh tundu lissu ambae alivamiwa na watu wasiojulikana na kupigwa risasi akiwa kwake dodoma

Patrobas kupitia mkutano na wandishi wa habari 23 sep alisema kama polisi watashindwa kuwapata wanaowaita wasiojulikana tutawatafuta wasiojulikana kwa njia zisizo jilikana na tutukigundua kuwa asiejulikana ndie asie julikana tutamshugurikia kwa njia zisizo julikana

Lkn kiongozi huyo leo yuko chama cha mapinduzi ccm je tuamin kuwa hii ndio njia isiojulikana aloichukua katambi ya kuwatafuta wasiojulikana au ule mpango wake wa kuwatafuta ameuahirisha je ninjaa? 

Maswali hayo msomaji waweza kujiuliza ukakosa majibu ya kueleweka zaidi zaidi utabaki kuvishauri vyama vya siasa kuwa viwe makini sana na watu wanaowapokea

Wengi hoja zao ni kuunga mkono jitihada ya dhati alonayo rais wetu john pombe magufuri wakati wengine wanasema wanataka kupigania demokrasia ya kwel.

Je tumuamini nani na nani tusimuamin wakati huo kumbuka tayari tumekalilishwa kuwa siasa ni mchezo mchafu

B

Comments

Popular posts from this blog

NYOTA YA MZALIWA WA KWANZA

SANAA NI NINI?

STORY YA UTAKE