BOKO HARAMU WAPIGA RISASI NA KUWACHINJA WATU

BOKO HARAMU 
Watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa Boko Haram, wamewapiga risasi na kuwachinja watu katika vijiji vitatu Kaskazini Mashariki ya Nigeria licha ya serikali kudai mwishoni mwa wiki kuwa ilifikia makubaliano na kundi hilo.
Wapiganaji wa Boko Haram, walivamia vijiji viwili Jumamosi na kupandisha bendera yao kwa mara ya tatu. Hii ni kwa mujibu wa wanakijiji wa eneo hilo.
Serikali ilisema kuwa itaendelea kufanya mazungumzo na Boko Haram licha ya madai ya kundi hilo kuvunja makubaliano.
Inatumai kuwa kundi hilo litawaachilia zaidi ya wasichana miambili waliowateka nyara amwezi Aprili.
Boko Haram hawajasema chochote kuhusu tamko la serikali ya Nigeria Ijumaa kwamba wamekubali kusitisha vita na kuwaachilia wanafunzi hao miambaili waliotekwa nyara katika eneo la Chibok.

Comments

Popular posts from this blog

NYOTA YA MZALIWA WA KWANZA

SANAA NI NINI?

STORY YA UTAKE